Wednesday, October 10, 2012

Facial Mask ya parachichi,asali,mtindi na limao



Vinavyohitajika:
1.Avocado moja lililoiva vyema.



2.Mtindi kijiko kimoja cha chakula.




3.Asali asilia (natural honey).



4.Maji ya ndimu/limao.




Namna ya kutayarisha:
Kata Avocado katika vipande viwili, ondoa kokwa na menya.
Changanya avocado ulomenya na mtindi, asali na maji ya ndimu au limao. Koroga mapaka upate mchanganyiko wa hali moja halafu weka pembeni.
Chukua maganda ya avocado na kwa upande wa ndani ya maganda hayo sugulia uso na shingo. Kufanya hivyo husaidia kuondoa seli zilizokufa na ngozi zilizoharibika. Pia huutayarisha uso kwa ajili ya mask.
Kisha paka mchanganyiko uliotayarisha usoni na shingoni (sio machoni).
Subiri kwa dakika 15 na kisha osha kwa maji vuguvugu.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.